-
Waebrania 9:11, 12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Hata hivyo, Kristo alipokuja akiwa kuhani mkuu wa mambo mema ambayo tayari yamefanyika, aliingia katika hema kubwa na kamilifu zaidi ambalo halikutengenezwa kwa mikono, yaani, si la uumbaji huu. 12 Aliingia mahali patakatifu, si kwa damu ya mbuzi na ya ng’ombe dume wachanga, bali kwa damu yake mwenyewe,+ mara moja kwa wakati wote, na kupata ukombozi wa* milele kwa ajili yetu.+
-
-
Waebrania 10:8-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Kwanza aliposema: “Hukutaka wala hukukubali dhabihu, matoleo, dhabihu nzima za kuteketezwa, na dhabihu za dhambi”—dhabihu zinazotolewa kulingana na Sheria— 9 kisha anasema: “Tazama! nimekuja kufanya mapenzi yako.”+ Anaondoa la kwanza ili asimamishe la pili. 10 Kwa “mapenzi” hayo+ sisi tumetakaswa kupitia toleo la mwili wa Yesu Kristo mara moja kwa wakati wote.+
-