-
Danieli 4:18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 “‘Hiyo ndiyo ndoto ambayo mimi, Mfalme Nebukadneza, niliota; sasa, Ee Belteshaza, nieleze maana ya ndoto hiyo, kwa maana wanaume wengine wote wenye hekima katika ufalme wangu wameshindwa kunieleza maana yake.+ Lakini wewe unaweza kufanya hivyo, kwa sababu roho ya miungu mitakatifu imo ndani yako.’
-
-
Danieli 5:11, 12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Kuna mwanamume fulani* katika ufalme wako aliye na roho ya miungu mitakatifu. Katika siku za baba yako, mwanamume huyo alithibitika kuwa na ujuzi na ufahamu na hekima kama hekima ya miungu.+ Baba yako Mfalme Nebukadneza alimweka kuwa mkuu wa makuhani wachawi, watu wanaofanya mazingaombwe, Wakaldayo,* na wanajimu;+ hivyo ndivyo alivyofanya baba yako, Ee mfalme. 12 Kwa maana Danieli, ambaye mfalme alimwita Belteshaza,+ alikuwa na roho isiyo ya kawaida na ujuzi na ufahamu wa kueleza maana ya ndoto, kufumbua mafumbo, na kutatua matatizo magumu.*+ Basi agiza Danieli aitwe, atakwambia maana ya maandishi haya.”
-