-
Waamuzi 20:4-6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Kwa hiyo yule Mlawi,+ mume wa mwanamke aliyeuawa, akajibu: “Mimi na suria wangu tulifika Gibea+ katika nchi ya Wabenjamini ili tulale usiku. 5 Kisha wakaaji* wa Gibea wakaja kunishambulia na kuizingira nyumba usiku. Walitaka kuniua, lakini wakambaka suria wangu, naye akafa.+ 6 Basi nikachukua maiti ya suria wangu na kuikatakata vipandevipande, kisha nikavipeleka vipande hivyo katika maeneo* yote ya urithi ya Waisraeli,+ kwa sababu walitenda jambo la aibu na lenye kufedhehesha katika Israeli.
-