Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 7:6-8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Kwa maana ninyi ni watu watakatifu kwa Yehova Mungu wenu, na Yehova Mungu wenu amewachagua ninyi muwe watu wake, mali yake ya pekee,* kutoka kati ya mataifa yote yaliyo duniani.+

      7 “Yehova hakuwapenda na kuwachagua ninyi eti kwa sababu mlikuwa wengi kuliko mataifa yote,+ kwa maana mlikuwa taifa dogo zaidi kati ya mataifa yote.+ 8 Badala yake, ni kwa sababu Yehova anawapenda na alitimiza kiapo alichowaapia mababu zenu,+ ndiyo maana Yehova aliwatoa Misri kwa mkono wake wenye nguvu na kuwakomboa kutoka katika nyumba ya utumwa,+ kutoka katika nguvu za* Farao mfalme wa Misri.

  • 2 Wafalme 13:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Hata hivyo, Yehova akawaonyesha kibali na rehema+ na kuwajali kwa sababu ya agano lake na Abrahamu,+ Isaka,+ na Yakobo.+ Hakutaka kuwaangamiza, naye hajawatupa mbali kutoka mbele zake* mpaka leo.

  • Zaburi 106:44, 45
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 44 Lakini alikuwa akiona taabu yao+

      Na kusikia kilio chao cha kuomba msaada.+

      45 Na kwa ajili yao alikuwa akikumbuka agano lake,

      Naye alikuwa akiwahurumia,* akichochewa na upendo wake mwingi* mshikamanifu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki