-
2 Wafalme 10:29-31Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
29 Hata hivyo, Yehu hakugeuka na kuacha dhambi ambazo Yeroboamu mwana wa Nebati alisababisha Waisraeli kutenda kuhusiana na wale ndama wa dhahabu waliokuwa Betheli na Dani.+ 30 Basi Yehova akamwambia Yehu: “Kwa kuwa umetenda vema na umefanya yaliyo sawa machoni pangu kwa kutenda mambo yote yaliyokuwa moyoni mwangu niliyokusudia kuitendea nyumba ya Ahabu,+ vizazi vinne vya wana wako vitaketi kwenye kiti cha ufalme cha Israeli.”+ 31 Lakini Yehu hakuwa mwangalifu kutembea katika Sheria ya Yehova Mungu wa Israeli kwa moyo wake wote.+ Hakugeuka na kuacha dhambi ambazo Yeroboamu alisababisha Waisraeli kutenda.+
-