9 Shangilia sana, Ee binti ya Sayuni.
Paza sauti kwa ushindi, Ee binti ya Yerusalemu.
Tazama! Mfalme wako anakuja kwako.+
Yeye ni mwadilifu, analeta wokovu,
Ni mnyenyekevu+ na amepanda punda,
Amepanda mwanapunda dume, mwana wa punda jike.+
10 Nitaondoa gari la vita Efraimu
Na farasi kutoka Yerusalemu.
Upinde wa vita utachukuliwa.
Naye atatangaza amani kwa mataifa;+
Utawala wake utaenea kutoka bahari mpaka bahari
Na kutoka Mto Efrati mpaka kwenye miisho ya dunia.+