6 Yehova anasema hivi:
‘“Kwa sababu ya maasi matatu ya Gaza,+ na hata manne, sitabadili uamuzi wangu,
Kwa sababu walichukua kundi lote la mateka+ na kuwatia mikononi mwa Edomu.
7 Basi nitaushushia moto ukuta wa Gaza,+
Nao utateketeza kabisa minara yake yenye ngome.
8 Nitawaangamiza wakaaji wa Ashdodi,+
Na mtawala wa Ashkeloni;+
Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni,+
Na Wafilisti wanaobaki wataangamia,”+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.’