Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 2:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Ndiyo sababu mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana* na mke wake, nao watakuwa mwili mmoja.+

  • Mathayo 5:32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Hata hivyo, ninawaambia kila mtu anayemtaliki mke wake kwa sababu nyingine isipokuwa uasherati,* anamweka katika kishawishi cha kufanya uzinzi, na yeyote anayemwoa mwanamke aliyetalikiwa anafanya uzinzi.+

  • Mathayo 19:8, 9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Akawajibu: “Musa aliwaruhusu kuwataliki wake zenu kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu,+ lakini haikuwa hivyo tangu mwanzo.+ 9 Ninawaambia kwamba mtu yeyote anayemtaliki mke wake isipokuwa kwa sababu ya uasherati,* na kumwoa mwingine, anafanya uzinzi.”+

  • Marko 10:5-9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Lakini Yesu akawaambia: “Aliwaandikia amri hiyo+ kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.+ 6 Hata hivyo, tangu mwanzo wa uumbaji ‘Aliwaumba mwanamume na mwanamke.+ 7 Kwa sababu hiyo, mwanamume atamwacha baba yake na mama yake,+ 8 na hao wawili watakuwa mwili mmoja,’+ basi wao si wawili tena, bali mwili mmoja. 9 Kwa hiyo, kile ambacho Mungu ameunganisha, mtu yeyote asikitenganishe.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki