14 Nanyi mnauliza, ‘Kwa sababu gani?’ Ni kwa sababu Yehova amekuwa shahidi kati yako na mke wa ujana wako, ambaye umemtendea kwa hila, ingawa yeye ni mwenzi wako na mke wako kupitia agano.*+
32 Hata hivyo, ninawaambia kila mtu anayemtaliki mke wake kwa sababu nyingine isipokuwa uasherati,* anamweka katika kishawishi cha kufanya uzinzi, na yeyote anayemwoa mwanamke aliyetalikiwa anafanya uzinzi.+
11 Akawaambia: “Yeyote anayemtaliki mke wake na kumwoa mwingine anafanya uzinzi+ dhidi yake, 12 na ikiwa mwanamke baada ya kumtaliki mume wake anaolewa na mwingine, anafanya uzinzi.”+
3 Hivyo basi, mume wake akiwa hai, mwanamke huyo ataitwa mzinzi ikiwa atakuwa wa mwanamume mwingine.+ Lakini mume wake akifa, yuko huru kutoka kwa sheria ya mume, basi mwanamke huyo si mzinzi ikiwa ataolewa na mwanamume mwingine.+