-
Luka 7:1-9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 Alipomaliza kuzungumza na watu, akaingia Kapernaumu. 2 Ofisa fulani wa jeshi alikuwa na mtumwa aliyempenda sana, na ambaye alikuwa mgonjwa sana karibu kufa.+ 3 Aliposikia kuhusu Yesu, akawatuma wazee fulani wa Wayahudi wamwombe Yesu aje kumponya mtumwa wake. 4 Walipofika kwa Yesu wakamsihi sana wakisema: “Mfanyie jambo hilo, anastahili 5 kwa maana analipenda taifa letu na yeye ndiye aliyetujengea sinagogi.” 6 Basi Yesu akaenda pamoja nao. Alipokaribia nyumba hiyo, yule ofisa wa jeshi alikuwa tayari amewatuma rafiki zake wamwambie: “Bwana, usijisumbue, kwa maana mimi sistahili uingie ndani ya nyumba yangu.+ 7 Ndiyo sababu niliona sistahili kuja kwako. Lakini sema tu neno, na mtumishi wangu atapona. 8 Kwa maana mimi pia niko chini ya mamlaka, na nina wanajeshi walio chini yangu, nami humwambia mmoja, ‘Nenda!’ naye huenda, na mwingine, ‘Njoo!’ naye huja, na mtumwa wangu, ‘Fanya hili!’ naye hulifanya.” 9 Yesu aliposikia maneno hayo alishangazwa naye, akaugeukia umati uliokuwa ukimfuata na kusema: “Ninawaambia, hata katika Israeli sijaona imani kubwa kama hii.”+
-