-
Luka 7:31-35Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
31 “Basi, nitawalinganisha watu wa kizazi hiki na nani, wanafanana na nani?+ 32 Wao ni kama watoto walioketi sokoni ambao wanaambiana kwa sauti kubwa, wakisema: ‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamkucheza dansi; tuliomboleza, lakini hamkulia.’ 33 Vivyo hivyo, Yohana Mbatizaji hakuja akila mkate wala kunywa divai,+ lakini mnasema: ‘Ana roho mwovu.’ 34 Mwana wa binadamu amekuja akila na kunywa, lakini mnasema: ‘Tazama! yeye ni mlafi na mwenye mazoea ya kunywa divai, rafiki ya wakusanya kodi na watenda dhambi!’+ 35 Hata hivyo, hekima huthibitishwa* kuwa yenye uadilifu kupitia watoto wake wote.”*+
-