-
Marko 7:8-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Mnaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo ya wanadamu.”+
9 Akaendelea kuwaambia: “Mnapuuza amri ya Mungu kwa ujanja ili mfuate mapokeo yenu.+ 10 Kwa mfano, Musa alisema, ‘Mheshimu baba yako na mama yako,’+ na, ‘Yeyote anayemtukana* baba yake au mama yake anapaswa kuuawa.’+ 11 Lakini ninyi mnasema, ‘Mtu akimwambia baba yake au mama yake: “Chochote nilicho nacho ambacho kingekusaidia ni korbani, (yaani, zawadi iliyowekwa wakfu kwa Mungu),”’ 12 hivyo mnamzuia kumsaidia kwa chochote baba yake au mama yake.+ 13 Kwa hiyo, mnalibatilisha neno la Mungu kwa mapokeo yenu ambayo mlipewa.+ Nanyi mnafanya mambo mengine mengi kama hayo.”+
-