Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 9:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Yesu alipokuwa akitoka huko, wanaume wawili vipofu+ wakamfuata, wakipaza sauti: “Tuhurumie,* Mwana wa Daudi.”

  • Marko 10:46-52
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 46 Kisha wakafika Yeriko. Lakini yeye na wanafunzi wake na umati mkubwa walipokuwa wakitoka Yeriko, Bartimayo (mwana wa Timayo), kipofu aliyekuwa akiombaomba, alikuwa ameketi kando ya barabara.+ 47 Aliposikia kwamba ni Yesu Mnazareti, akaanza kusema kwa sauti kubwa: “Mwana wa Daudi,+ Yesu, nihurumie!”*+ 48 Ndipo wengi wakaanza kumkemea, wakimwambia anyamaze, lakini akazidi kusema kwa sauti kubwa: “Mwana wa Daudi, nihurumie!”* 49 Basi Yesu akasimama na kusema: “Mwiteni.” Nao wakamwita yule kipofu, wakamwambia: “Jipe moyo! Simama; anakuita.” 50 Akatupa vazi lake la nje, akasimama haraka na kumwendea Yesu. 51 Kisha Yesu akamwuliza: “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akamwambia: “Raboni,* naomba niweze kuona tena.” 52 Yesu akamwambia: “Nenda, imani yako imekuponya.”+ Na mara moja akaanza kuona,+ naye akaanza kumfuata barabarani.

  • Luka 18:35-43
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 Yesu alipokaribia Yeriko kipofu mmoja alikuwa ameketi kando ya barabara akiombaomba.+ 36 Aliposikia umati ukipita, akaanza kuuliza kilichokuwa kikiendelea. 37 Wakamjibu: “Yesu Mnazareti ndiye anayepita!”⁠ 38 Ndipo akasema kwa sauti kubwa: “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”* 39 Wale waliokuwa mbele wakaanza kumkemea wakimwambia anyamaze, lakini akazidi kusema kwa sauti kubwa: “Mwana wa Daudi, nihurumie!”* 40 Kisha Yesu akasimama na kuagiza mtu huyo aletwe kwake. Alipokaribia, Yesu akamuuliza: 41 “Unataka nikufanyie nini?” Akasema: “Bwana, naomba niweze kuona tena.” 42 Basi Yesu akamwambia: “Ona tena; imani yako imekuponya.”+ 43 Mara moja akaanza kuona tena, naye akaanza kumfuata Yesu+ huku akimtukuza Mungu. Pia, watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki