-
Marko 10:46-52Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
46 Kisha wakafika Yeriko. Lakini yeye na wanafunzi wake na umati mkubwa walipokuwa wakitoka Yeriko, Bartimayo (mwana wa Timayo), kipofu aliyekuwa akiombaomba, alikuwa ameketi kando ya barabara.+ 47 Aliposikia kwamba ni Yesu Mnazareti, akaanza kusema kwa sauti kubwa: “Mwana wa Daudi,+ Yesu, nihurumie!”*+ 48 Ndipo wengi wakaanza kumkemea, wakimwambia anyamaze, lakini akazidi kusema kwa sauti kubwa: “Mwana wa Daudi, nihurumie!”* 49 Basi Yesu akasimama na kusema: “Mwiteni.” Nao wakamwita yule kipofu, wakamwambia: “Jipe moyo! Simama; anakuita.” 50 Akatupa vazi lake la nje, akasimama haraka na kumwendea Yesu. 51 Kisha Yesu akamwuliza: “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akamwambia: “Raboni,* naomba niweze kuona tena.” 52 Yesu akamwambia: “Nenda, imani yako imekuponya.”+ Na mara moja akaanza kuona,+ naye akaanza kumfuata barabarani.
-
-
Luka 18:35-43Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
35 Yesu alipokaribia Yeriko kipofu mmoja alikuwa ameketi kando ya barabara akiombaomba.+ 36 Aliposikia umati ukipita, akaanza kuuliza kilichokuwa kikiendelea. 37 Wakamjibu: “Yesu Mnazareti ndiye anayepita!” 38 Ndipo akasema kwa sauti kubwa: “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”* 39 Wale waliokuwa mbele wakaanza kumkemea wakimwambia anyamaze, lakini akazidi kusema kwa sauti kubwa: “Mwana wa Daudi, nihurumie!”* 40 Kisha Yesu akasimama na kuagiza mtu huyo aletwe kwake. Alipokaribia, Yesu akamuuliza: 41 “Unataka nikufanyie nini?” Akasema: “Bwana, naomba niweze kuona tena.” 42 Basi Yesu akamwambia: “Ona tena; imani yako imekuponya.”+ 43 Mara moja akaanza kuona tena, naye akaanza kumfuata Yesu+ huku akimtukuza Mungu. Pia, watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.+
-