-
Luka 4:1-4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Basi Yesu, akiwa amejaa roho takatifu, akaondoka Yordani, naye akaongozwa na roho kwenda nyikani+ 2 kwa siku 40, akijaribiwa na Ibilisi.+ Kipindi hicho chote hakula chakula, basi muda huo ulipokwisha, akahisi njaa. 3 Ndipo Ibilisi akamwambia: “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, liambie jiwe hili liwe mkate.” 4 Lakini Yesu akamjibu: “Imeandikwa, ‘Mwanadamu hataishi kwa mkate tu.’”+
-