-
Mathayo 4:1-4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Ndipo Yesu akaongozwa na roho kuingia nyikani ili akajaribiwe+ na Ibilisi.+ 2 Baada ya kufunga kwa siku 40, mchana na usiku, akahisi njaa. 3 Naye Mjaribu+ akaja na kumwambia: “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, yaambie mawe haya yawe mikate.” 4 Lakini akajibu: “Imeandikwa: ‘Mwanadamu hataishi kwa mkate tu, bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Yehova.’”*+
-