-
Mathayo 4:1-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Ndipo Yesu akaongozwa na roho kuingia nyikani ili akajaribiwe+ na Ibilisi.+ 2 Baada ya kufunga kwa siku 40, mchana na usiku, akahisi njaa. 3 Naye Mjaribu+ akaja na kumwambia: “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, yaambie mawe haya yawe mikate.” 4 Lakini akajibu: “Imeandikwa: ‘Mwanadamu hataishi kwa mkate tu, bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Yehova.’”*+
5 Ndipo Ibilisi akampeleka kwenye lile jiji takatifu,+ akamsimamisha juu ya mnara* wa hekalu+ 6 na kumwambia: “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, jitupe chini, kwa maana imeandikwa: ‘Atawaagiza malaika zake kukuhusu wewe,’ nao ‘Watakubeba mikononi mwao, ili mguu wako usigonge jiwe.’”+ 7 Yesu akamwambia: “Tena imeandikwa: ‘Usimjaribu Yehova* Mungu wako.’”+
8 Tena Ibilisi akampeleka Yesu kwenye mlima mrefu sana, akamwonyesha falme zote za ulimwengu na utukufu wazo.+ 9 Naye akamwambia: “Nitakupa vitu hivi vyote ukianguka chini na kunifanyia tendo la ibada.” 10 Ndipo Yesu akamwambia: “Nenda zako, Shetani! Kwa maana imeandikwa: ‘Yehova* Mungu wako ndiye unayepaswa kumwabudu,+ na yeye peke yake ndiye unayepaswa kumtolea utumishi mtakatifu.’”+
-
-
Luka 4:1-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Basi Yesu, akiwa amejaa roho takatifu, akaondoka Yordani, naye akaongozwa na roho kwenda nyikani+ 2 kwa siku 40, akijaribiwa na Ibilisi.+ Kipindi hicho chote hakula chakula, basi muda huo ulipokwisha, akahisi njaa. 3 Ndipo Ibilisi akamwambia: “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, liambie jiwe hili liwe mkate.” 4 Lakini Yesu akamjibu: “Imeandikwa, ‘Mwanadamu hataishi kwa mkate tu.’”+
5 Basi akampeleka juu na kumwonyesha mara moja falme zote za dunia inayokaliwa.+ 6 Kisha Ibilisi akamwambia: “Nitakupa mamlaka yote hii na utukufu wake, kwa sababu nimepewa,+ nami humpa yeyote ninayetaka. 7 Kwa hiyo, ukifanya tendo la ibada mbele yangu, yote itakuwa yako.” 8 Yesu akamjibu: “Imeandikwa, ‘Yehova* Mungu wako ndiye unayepaswa kumwabudu na yeye peke yake ndiye unayepaswa kumtolea utumishi mtakatifu.’”+
9 Kisha akampeleka Yerusalemu, akamsimamisha juu ya mnara wa* hekalu na kumwambia: “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa,+ 10 kwa maana imeandikwa, ‘Atawaagiza malaika zake kukuhusu wewe, ili wakulinde,’ 11 nao, ‘Watakubeba mikononi mwao, ili mguu wako usigonge jiwe.’”+ 12 Yesu akamjibu: “Imesemwa, ‘Usimjaribu Yehova* Mungu wako.’”+ 13 Kwa hiyo Ibilisi, alipomaliza majaribu yote, akamwacha mpaka wakati mwingine unaofaa.+
-