21 Tangu wakati huo, Yesu akaanza kuwafafanulia wanafunzi wake kwamba ni lazima aende Yerusalemu na kuteswa sana na wazee, wakuu wa makuhani, na waandishi, kisha atauawa, na siku ya tatu afufuliwe.+
22 Walipokuwa wamekusanyika huko Galilaya, Yesu akawaambia: “Mwana wa binadamu atasalitiwa mikononi mwa watu,+23 nao watamuua, na siku ya tatu atafufuliwa.”+ Kwa hiyo wakahuzunika sana.
3 Kwa maana kati ya mambo ya kwanza niliyowapa ni yale niliyopokea pia, kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kulingana na Maandiko;+4 na kwamba alizikwa,+ ndiyo, kwamba alifufuliwa+ siku ya tatu+ kulingana na Maandiko;+