22 Walipokuwa wamekusanyika huko Galilaya, Yesu akawaambia: “Mwana wa binadamu atasalitiwa mikononi mwa watu,+23 nao watamuua, na siku ya tatu atafufuliwa.”+ Kwa hiyo wakahuzunika sana.
18 “Tazama! Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa binadamu atatiwa mikononi mwa wakuu wa makuhani na waandishi. Nao watamhukumia kifo+19 na kumtia mikononi mwa watu wa mataifa ili wamdhihaki, wampige mijeledi, na kumuua kwenye mti;+ na siku ya tatu atafufuliwa.”+
31 Pia, akaanza kuwafundisha kwamba Mwana wa binadamu lazima apatwe na mateso mengi na kukataliwa na wazee, wakuu wa makuhani, na waandishi, kisha atauawa,+ na baada ya siku tatu atafufuliwa.+
22 lakini akasema: “Lazima Mwana wa binadamu apatwe na mateso mengi, akataliwe na wazee, wakuu wa makuhani, na waandishi, kisha atauawa,+ na siku ya tatu atafufuliwa.”+
3 Kwa maana kati ya mambo ya kwanza niliyowapa ni yale niliyopokea pia, kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kulingana na Maandiko;+4 na kwamba alizikwa,+ ndiyo, kwamba alifufuliwa+ siku ya tatu+ kulingana na Maandiko;+