Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 16:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kwa maana hutaniacha* Kaburini.*+

      Hutamruhusu mshikamanifu wako aone shimo.*+

  • Isaya 53:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Kwa sababu hiyo nitampa fungu kati ya wengi,

      Naye atagawa nyara pamoja na wenye nguvu,

      Kwa sababu aliumwaga uhai wake* mpaka kifo+

      Naye alihesabiwa miongoni mwa wakosaji;+

      Aliibeba dhambi ya watu wengi,+

      Naye aliwatetea wakosaji.+

  • Mathayo 17:22, 23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Walipokuwa wamekusanyika huko Galilaya, Yesu akawaambia: “Mwana wa binadamu atasalitiwa mikononi mwa watu,+ 23 nao watamuua, na siku ya tatu atafufuliwa.”+ Kwa hiyo wakahuzunika sana.

  • Mathayo 20:18, 19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 “Tazama! Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa binadamu atatiwa mikononi mwa wakuu wa makuhani na waandishi. Nao watamhukumia kifo+ 19 na kumtia mikononi mwa watu wa mataifa ili wamdhihaki, wampige mijeledi, na kumuua kwenye mti;+ na siku ya tatu atafufuliwa.”+

  • Marko 8:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Pia, akaanza kuwafundisha kwamba Mwana wa binadamu lazima apatwe na mateso mengi na kukataliwa na wazee, wakuu wa makuhani, na waandishi, kisha atauawa,+ na baada ya siku tatu atafufuliwa.+

  • Luka 9:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 lakini akasema: “Lazima Mwana wa binadamu apatwe na mateso mengi, akataliwe na wazee, wakuu wa makuhani, na waandishi, kisha atauawa,+ na siku ya tatu atafufuliwa.”+

  • Luka 24:46
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 46 naye akawaambia: “Imeandikwa kwamba Kristo atateseka na kufufuliwa kutoka kwa wafu siku ya tatu,+

  • 1 Wakorintho 15:3, 4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Kwa maana kati ya mambo ya kwanza niliyowapa ni yale niliyopokea pia, kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu kulingana na Maandiko;+ 4 na kwamba alizikwa,+ ndiyo, kwamba alifufuliwa+ siku ya tatu+ kulingana na Maandiko;+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki