5 Kwa maana kuna Mungu mmoja,+ na mpatanishi mmoja+ kati ya Mungu na wanadamu,+ mwanadamu, Kristo Yesu,+6 aliyejitoa kuwa fidia inayolingana kwa ajili ya wote*+—hilo litatolewa ushahidi kwa wakati wake unaofaa.
13 huku tukingojea tumaini lenye furaha+ na kufunuliwa kwenye utukufu kwa Mungu mkuu na kwa Mwokozi wetu, Yesu Kristo, 14 aliyejitoa kwa ajili yetu+ ili atuweke huru*+ kutoka katika kila namna ya uasi sheria na kujisafishia watu walio mali yake ya pekee, wenye bidii katika matendo mema.+
28 vivyo hivyo pia Kristo alitolewa mara moja kwa wakati wote ili kubeba dhambi za wengi;+ na mara ya pili atakapotokea itakuwa bila dhambi,* naye ataonwa na wale wanaomtazamia kwa bidii kwa ajili ya wokovu wao.+