26 Wakafika pwani ya eneo la Wagerasene,+ lililo ng’ambo ya Galilaya. 27 Yesu alipotoka kwenye mashua akakutana na mwanamume fulani kutoka jijini aliyekuwa na roho mwovu. Hakuwa amevaa nguo kwa muda mrefu, na hakuwa akiishi katika nyumba bali aliishi makaburini.+