-
Mathayo 8:28, 29Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
28 Alipofika upande ule mwingine na kuingia katika eneo la Wagadarene, alikutana na wanaume wawili waliokuwa na roho waovu wakitoka makaburini.*+ Walikuwa wakali sana, hivi kwamba hakuna mtu aliyekuwa na ujasiri wa kupita katika barabara hiyo. 29 Na tazama! wakapiga mayowe wakisema: “Kwa nini unatusumbua, Mwana wa Mungu?+ Je, umekuja kututesa+ kabla ya wakati uliowekwa?”+
-
-
Marko 5:2-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Mara tu Yesu alipotoka kwenye mashua akakutana na mtu mwenye roho mwovu akitoka makaburini.* 3 Alikuwa akikaa makaburini, na kufikia wakati huo hakuna mtu yeyote aliyeweza kumfunga kabisa hata kwa mnyororo. 4 Alikuwa amefungwa mara nyingi kwa pingu na minyororo, lakini aliikata minyororo na kuzivunja pingu; na hakuna mtu aliyeweza kumzuia. 5 Sikuzote, usiku na mchana alikuwa akipaza sauti makaburini na milimani na kujikatakata kwa mawe. 6 Lakini alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia na kumwinamia.+ 7 Kisha akapaza sauti na kusema: “Kwa nini unanisumbua, Yesu, Mwana wa Mungu Aliye Juu Zaidi? Ninakuapisha kwa Mungu usinitese.”+ 8 Kwa maana Yesu alikuwa akimwambia: “Mtoke mtu huyu, wewe roho mwovu.”+ 9 Lakini Yesu akamuuliza: “Unaitwa nani?” Naye akamwambia: “Jina langu ni Kikosi, kwa sababu tuko wengi.” 10 Naye akamsihi sana Yesu asiwafukuze roho hao kutoka katika nchi hiyo.+
-