-
Mathayo 26:17-19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Siku ya kwanza ya Sherehe ya Mikate Isiyo na Chachu+ wanafunzi wakaja kumuuliza Yesu: “Unataka tukutayarishie wapi mlo wa Pasaka?”+ 18 Akawaambia: “Nendeni jijini kwa mwanamume fulani mkamwambie, ‘Mwalimu anasema: “Wakati wangu uliowekwa umekaribia; nitasherehekea Pasaka pamoja na wanafunzi wangu nyumbani kwako.”’” 19 Basi, wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaagiza, wakaandaa Pasaka.
-