-
Marko 14:12-16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Sasa siku ya kwanza ya Sherehe ya Mikate Isiyo na Chachu,+ wakati ambapo walikuwa na desturi ya kutoa dhabihu ya Pasaka,+ wanafunzi wake wakamwuliza: “Unataka twende tukutayarishie wapi mlo wa Pasaka?”+ 13 Ndipo akawatuma wawili kati ya wanafunzi wake akawaambia: “Nendeni jijini, nanyi mtakutana na mwanamume akiwa amebeba mtungi wa maji. Mfuateni,+ 14 na popote atakapoingia, mwambieni mwenye nyumba, ‘Mwalimu anasema: “Kiko wapi chumba cha wageni ambamo ninaweza kula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?”’ 15 Naye atawaonyesha chumba kikubwa cha juu, chenye vifaa na kilichotayarishwa. Tuandalieni humo.” 16 Basi wanafunzi wakaenda, wakaingia jijini na kupata kama alivyowaambia, nao wakaandaa Pasaka.
-
-
Luka 22:7-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 Siku ya Sherehe ya Mikate Isiyo na Chachu ikafika, siku ambayo dhabihu ya Pasaka hutolewa;+ 8 basi Yesu akawatuma Petro na Yohana, akawaambia: “Nendeni mkatutayarishie Pasaka tule.”+ 9 Wakamuuliza: “Unataka tuitayarishe wapi?” 10 Akawaambia: “Tazameni! Mtakapoingia jijini, mtakutana na mwanamume akiwa amebeba mtungi wa maji. Mfuateni mwingie katika nyumba atakayoingia.+ 11 Mwambieni mwenye nyumba hiyo, ‘Mwalimu anasema: “Kiko wapi chumba cha wageni ambamo ninaweza kula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?”’ 12 Mtu huyo atawaonyesha chumba kikubwa cha juu chenye vifaa. Tayarisheni humo.” 13 Basi wakaenda na kupata kama alivyokuwa amewaambia, nao wakaandaa Pasaka.
-