-
Mathayo 9:14, 15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 Kisha wanafunzi wa Yohana wakaja na kumuuliza: “Kwa nini sisi na Mafarisayo hufunga lakini wanafunzi wako hawafungi?”+ 15 Ndipo Yesu akawaambia: “Rafiki za bwana harusi hawahitaji kuomboleza bwana harusi+ anapokuwa pamoja nao, sivyo? Lakini siku zitakuja ambapo bwana harusi ataondolewa kwao,+ ndipo watakapofunga.
-
-
Luka 5:33-35Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
33 Wakamwambia: “Wanafunzi wa Yohana hufunga mara nyingi na kutoa dua, na pia wanafunzi wa Mafarisayo, lakini wanafunzi wako hula na kunywa.”+ 34 Yesu akawaambia: “Hamwezi kuwafanya rafiki za bwana harusi wafunge bwana harusi akiwa pamoja nao, sivyo? 35 Lakini siku zitakuja ambapo kwa kweli bwana harusi+ ataondolewa kwao; ndipo watakapofunga siku hizo.”+
-