-
Marko 2:18-20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Wanafunzi wa Yohana na Mafarisayo walikuwa na zoea la kufunga. Basi wakaja na kumuuliza Yesu: “Kwa nini wanafunzi wa Yohana na wanafunzi wa Mafarisayo hufunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?”+ 19 Yesu akawajibu: “Rafiki za bwana harusi+ hawahitaji kufunga wanapokuwa naye, sivyo? Bwana harusi akiwa pamoja nao hawawezi kufunga. 20 Lakini siku zitakuja ambapo bwana harusi ataondolewa kwao,+ ndipo watakapofunga siku hiyo.
-
-
Luka 5:33-35Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
33 Wakamwambia: “Wanafunzi wa Yohana hufunga mara nyingi na kutoa dua, na pia wanafunzi wa Mafarisayo, lakini wanafunzi wako hula na kunywa.”+ 34 Yesu akawaambia: “Hamwezi kuwafanya rafiki za bwana harusi wafunge bwana harusi akiwa pamoja nao, sivyo? 35 Lakini siku zitakuja ambapo kwa kweli bwana harusi+ ataondolewa kwao; ndipo watakapofunga siku hizo.”+
-