-
Mathayo 27:46-49Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
46 Karibu saa tisa, Yesu akapaza sauti, akisema: “Eli, Eli, lama sabakthani?” yaani, “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”+ 47 Waliposikia hilo, baadhi ya wale waliokuwa wamesimama hapo wakaanza kusema: “Mtu huyu anamwita Eliya.”+ 48 Mara moja, mmoja wao akakimbia, akachukua sifongo akailowesha katika divai kali akaiweka kwenye utete akampa anywe.+ 49 Lakini wengine wakasema: “Mwacheni! Acheni tuone kama Eliya atakuja kumwokoa.”
-