-
Mathayo 3:7-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 Alipoona Mafarisayo na Masadukayo+ wengi wakija kwenye ubatizo, akawaambia: “Enyi uzao wa nyoka,*+ ni nani amewaonya ili mkimbie ghadhabu inayokuja?+ 8 Basi zaeni matunda yanayoonyesha toba. 9 Msithubutu kujiambia, ‘Abrahamu ndiye baba yetu.’+ Kwa maana ninawaambia, Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka kwenye mawe haya. 10 Tayari shoka limewekwa kwenye mzizi wa miti. Basi, kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.+
-