-
Mathayo 9:2-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Na tazama! wakamletea mtu aliyepooza, akiwa amelala kwenye kitanda.* Alipoona imani yao, Yesu akamwambia yule mtu aliyepooza: “Jipe moyo mwanangu! Umesamehewa dhambi zako.”+ 3 Sasa baadhi ya waandishi wakaambiana: “Mtu huyu anakufuru.” 4 Yesu, akijua fikira zao, akasema: “Kwa nini mnawaza mambo maovu katika mioyo yenu?+ 5 Kwa mfano, ni jambo gani rahisi zaidi kusema, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Simama utembee’?+ 6 Hata hivyo, ili mjue kwamba Mwana wa binadamu ana mamlaka ya kusamehe dhambi duniani—” kisha akamwambia yule mtu aliyepooza: “Simama, chukua kitanda chako, uende nyumbani.”+ 7 Ndipo akasimama, akaenda nyumbani. 8 Umati ulipoona hivyo ukaogopa, nao wakamtukuza Mungu aliyewapa wanadamu mamlaka ya namna hiyo.
-