14 Walipofika karibu na umati,+ mtu fulani akamkaribia Yesu, akapiga magoti, na kusema: 15 “Bwana, mhurumie mwanangu, kwa sababu ana kifafa na ni mgonjwa sana. Yeye huanguka ndani ya moto na ndani ya maji mara nyingi.+ 16 Nilimleta kwa wanafunzi wako, lakini walishindwa kumponya.”