-
Mathayo 17:14-17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 Walipofika karibu na umati,+ mtu fulani akamkaribia Yesu, akapiga magoti, na kusema: 15 “Bwana, mhurumie* mwanangu, kwa sababu ana kifafa na ni mgonjwa sana. Yeye huanguka ndani ya moto na ndani ya maji mara nyingi.+ 16 Nilimleta kwa wanafunzi wako, lakini walishindwa kumponya.” 17 Yesu akajibu: “Enyi kizazi kisicho na imani na kilichopotoka,+ nitaendelea kuwa pamoja nanyi mpaka lini? Nitawavumilia mpaka lini? Mleteni hapa.”
-
-
Luka 9:38-42Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
38 Na tazama! mtu fulani katika umati akasema kwa sauti kubwa: “Mwalimu, ninakuomba umwangalie mwanangu, kwa sababu yeye ni mwanangu wa pekee.+ 39 Tazama! roho mwovu humshika, naye hupiga kelele ghafla, na humfanya agaegae na kutokwa na povu mdomoni, naye hamtoki upesi mpaka anapomjeruhi. 40 Niliwaomba wanafunzi wako wamfukuze, lakini wakashindwa.” 41 Yesu akajibu: “Enyi kizazi kisicho na imani na kilichopotoka,+ nitaendelea kuwa pamoja nanyi na kuwavumilia mpaka lini? Mlete mwanao hapa.”+ 42 Lakini alipokuwa akikaribia, yule roho mwovu akamwangusha na kumfanya agaegae sana. Hata hivyo, Yesu akamkemea yule roho mwovu na kumponya mvulana huyo, kisha akamkabidhi kwa baba yake.
-