-
1 Wathesalonike 2:14-16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 Kwa maana, akina ndugu mliiga makutaniko ya Mungu yaliyo katika muungano na Kristo Yesu huko Yudea, kwa sababu mliteswa na wananchi wenzenu,+ kama vile wao pia wanavyoteswa na Wayahudi, 15 ambao hata walimuua Bwana Yesu+ na manabii na wakatutesa.+ Zaidi ya hayo, hawafanyi mambo yanayompendeza Mungu, na wanapinga mambo yanayowafaa wanadamu wote, 16 wakijaribu kutuzuia kuzungumza na watu wa mataifa ili waokolewe.+ Kwa hiyo, sikuzote wanajaza kipimo cha dhambi zao. Lakini hatimaye hasira yake imekuja juu yao.+
-