19 Hata hivyo, mtakapopelekwa, msihangaike kuhusu jambo mtakalosema au jinsi mtakavyolisema, kwa sababu mtapewa jambo la kusema katika saa hiyo;+20 kwa maana si ninyi tu mnaosema, bali ni roho ya Baba yenu inayosema kupitia ninyi.+
11 Na watakapokuwa wakiwapeleka kuwashtaki, msihangaike kuhusu jambo mtakalosema; bali semeni jambo mtakalopewa saa hiyo, kwa maana si ninyi mnaosema, bali ni roho takatifu.+
14 Kwa hiyo, azimieni mioyoni mwenu kwamba hamtafanya mazoezi mapema kuhusu jinsi mtakavyojitetea,+15 kwa maana nitawapa maneno na hekima, ambayo wapinzani wenu wote kwa pamoja hawataweza kushindana nayo wala kubisha.+