Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 4:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Basi nenda sasa, nami nitakuwa pamoja nawe utakapokuwa ukizungumza,* nami nitakufundisha unalopaswa kusema.”+

  • Mathayo 10:19, 20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Hata hivyo, mtakapopelekwa, msihangaike kuhusu jambo mtakalosema au jinsi mtakavyolisema, kwa sababu mtapewa jambo la kusema katika saa hiyo;+ 20 kwa maana si ninyi tu mnaosema, bali ni roho ya Baba yenu inayosema kupitia ninyi.+

  • Luka 12:11, 12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Mtakapopelekwa mbele ya makusanyiko ya watu wote,* maofisa wa serikali, na mamlaka, msihangaike kuhusu jinsi mtakavyojitetea au jambo mtakalosema,+ 12 kwa maana saa hiyohiyo roho takatifu itawafundisha mambo mnayopaswa kusema.”+

  • Luka 21:14, 15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Kwa hiyo, azimieni mioyoni mwenu kwamba hamtafanya mazoezi mapema kuhusu jinsi mtakavyojitetea,+ 15 kwa maana nitawapa maneno na hekima, ambayo wapinzani wenu wote kwa pamoja hawataweza kushindana nayo wala kubisha.+

  • Matendo 4:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Ndipo Petro, akiwa amejaa roho takatifu,+ akawaambia:

      “Watawala wa watu na wazee,

  • Matendo 6:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Lakini watu fulani wa Sinagogi la Watu Waliowekwa Huru wakaja mbele, pamoja na Wakirene na Waaleksandria, na wengine kutoka Kilikia na Asia, ili kubishana na Stefano. 10 Lakini hawakuweza kumshinda kwa sababu ya hekima yake na roho iliyomwongoza kusema.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki