-
Mathayo 24:48-51Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
48 “Lakini ikiwa mtumwa huyo mwovu atasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu anakawia,’+ 49 naye aanze kuwapiga watumwa wenzake na kula na kunywa pamoja na walevi wa kupindukia, 50 bwana wa mtumwa huyo atakuja siku asiyotazamia na katika saa asiyoijua,+ 51 naye atamwadhibu kwa ukali sana na kumweka pamoja na wanafiki. Huko ndiko atalia na kusaga meno yake.+
-