20 Akawaambia: “Ni kwa sababu ya imani yenu ndogo. Kwa kweli ninawaambia, mkiwa na imani inayolingana na mbegu ya haradali, mtauambia mlima huu, ‘Ondoka hapa uende pale,’ nao utaondoka, na hakuna jambo litakalowashinda.”+
21 Yesu akawajibu: “Kwa kweli ninawaambia, mkiwa na imani nanyi msiwe na shaka, hamtafanya tu nilichoufanyia mtini huo, bali hata mkiuambia mlima huu, ‘Ng’oka, ukatupwe baharini,’ jambo hilo litatendeka.+
23 Kwa kweli ninawaambia mtu yeyote anayeuambia mlima huu, ‘Ng’oka, ukatupwe baharini,’ bila kuwa na shaka moyoni mwake lakini awe na imani kwamba yale anayosema yatatukia, itakuwa hivyo.+