24Yesu alipokuwa akitoka hekaluni, wanafunzi wake wakamkaribia na kumwonyesha majengo ya hekalu. 2 Akawaambia: “Je, mnaona vitu hivi vyote? Kwa kweli ninawaambia, hakuna jiwe litakaloachwa hapa juu ya jiwe lingine bila kuangushwa chini.”+
13Alipokuwa akitoka hekaluni mmoja wa wanafunzi wake akamwambia: “Mwalimu, ona! jinsi mawe na majengo haya yalivyo maridadi!”+2 Hata hivyo, Yesu akamwambia: “Unayaona majengo haya makubwa? Hakuna jiwe litakaloachwa hapa juu ya jiwe lingine bila kuangushwa chini.”+