-
Luka 9:46-48Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
46 Kisha wanafunzi wakaanza kubishana kuhusu aliyekuwa mkuu zaidi kati yao.+ 47 Yesu, akijua mawazo ya mioyo yao, akachukua mtoto na kumsimamisha kando yake, 48 akawaambia: “Yeyote anayempokea mtoto huyu kwa msingi wa jina langu ananipokea mimi pia, na yeyote anayenipokea, anampokea pia Yule aliyenituma.+ Kwa maana anayejiendesha kama mdogo zaidi kati yenu nyote ndiye mkuu.”+
-