-
Mathayo 18:1-5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Katika saa hiyo wanafunzi wakamkaribia Yesu na kumuuliza: “Kwa kweli ni nani aliye mkuu zaidi katika Ufalme wa mbinguni?”+ 2 Basi akamwita mtoto mdogo, akamsimamisha katikati yao 3 na kusema: “Kwa kweli ninawaambia, msipogeuka* na kuwa kama watoto wadogo,+ hamtaingia kamwe katika Ufalme wa mbinguni.+ 4 Kwa hiyo, yeyote atakayejinyenyekeza kama mtoto huyu mdogo ndiye mkuu zaidi katika Ufalme wa mbinguni;+ 5 na yeyote anayempokea mtoto mdogo kama huyu kwa msingi wa jina langu ananipokea mimi pia.
-
-
Marko 9:33-37Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
33 Nao wakaingia Kapernaumu. Alipokuwa ndani ya nyumba akawauliza: “Mlikuwa mkibishania nini barabarani?”+ 34 Wakakaa kimya, kwa maana barabarani walikuwa wakibishana kuhusu aliye mkuu kati yao. 35 Basi akaketi na kuwaita wale 12 akawaambia: “Yeyote anayetaka kuwa wa kwanza, lazima awe wa mwisho kati ya wote na mhudumu wa wote.”+ 36 Kisha akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha katikati yao; akamkumbatia na kuwaambia: 37 “Yeyote anayempokea mtoto mdogo+ kama huyu kwa msingi wa jina langu ananipokea mimi pia; na yeyote anayenipokea mimi hanipokei mimi tu, bali pia Yule aliyenituma.”+
-