-
Marko 9:33-37Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
33 Nao wakaingia Kapernaumu. Alipokuwa ndani ya nyumba akawauliza: “Mlikuwa mkibishania nini barabarani?”+ 34 Wakakaa kimya, kwa maana barabarani walikuwa wakibishana kuhusu aliye mkuu kati yao. 35 Basi akaketi na kuwaita wale 12 akawaambia: “Yeyote anayetaka kuwa wa kwanza, lazima awe wa mwisho kati ya wote na mhudumu wa wote.”+ 36 Kisha akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha katikati yao; akamkumbatia na kuwaambia: 37 “Yeyote anayempokea mtoto mdogo+ kama huyu kwa msingi wa jina langu ananipokea mimi pia; na yeyote anayenipokea mimi hanipokei mimi tu, bali pia Yule aliyenituma.”+
-
-
Luka 9:46-48Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
46 Kisha wanafunzi wakaanza kubishana kuhusu aliyekuwa mkuu zaidi kati yao.+ 47 Yesu, akijua mawazo ya mioyo yao, akachukua mtoto na kumsimamisha kando yake, 48 akawaambia: “Yeyote anayempokea mtoto huyu kwa msingi wa jina langu ananipokea mimi pia, na yeyote anayenipokea, anampokea pia Yule aliyenituma.+ Kwa maana anayejiendesha kama mdogo zaidi kati yenu nyote ndiye mkuu.”+
-