Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Marko 9:33-37
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 33 Nao wakaingia Kapernaumu. Alipokuwa ndani ya nyumba akawauliza: “Mlikuwa mkibishania nini barabarani?”+ 34 Wakakaa kimya, kwa maana barabarani walikuwa wakibishana kuhusu aliye mkuu kati yao. 35 Basi akaketi na kuwaita wale 12 akawaambia: “Yeyote anayetaka kuwa wa kwanza, lazima awe wa mwisho kati ya wote na mhudumu wa wote.”+ 36 Kisha akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha katikati yao; akamkumbatia na kuwaambia: 37 “Yeyote anayempokea mtoto mdogo+ kama huyu kwa msingi wa jina langu ananipokea mimi pia; na yeyote anayenipokea mimi hanipokei mimi tu, bali pia Yule aliyenituma.”+

  • Luka 9:46-48
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 46 Kisha wanafunzi wakaanza kubishana kuhusu aliyekuwa mkuu zaidi kati yao.+ 47 Yesu, akijua mawazo ya mioyo yao, akachukua mtoto na kumsimamisha kando yake, 48 akawaambia: “Yeyote anayempokea mtoto huyu kwa msingi wa jina langu ananipokea mimi pia, na yeyote anayenipokea, anampokea pia Yule aliyenituma.+ Kwa maana anayejiendesha kama mdogo zaidi kati yenu nyote ndiye mkuu.”+

  • Luka 22:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Hata hivyo, pia kukatokea bishano kali kuhusu ni nani aliyekuwa mkuu zaidi kati yao.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki