Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 18:1-5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Katika saa hiyo wanafunzi wakamkaribia Yesu na kumuuliza: “Kwa kweli ni nani aliye mkuu zaidi katika Ufalme wa mbinguni?”+ 2 Basi akamwita mtoto mdogo, akamsimamisha katikati yao 3 na kusema: “Kwa kweli ninawaambia, msipogeuka* na kuwa kama watoto wadogo,+ hamtaingia kamwe katika Ufalme wa mbinguni.+ 4 Kwa hiyo, yeyote atakayejinyenyekeza kama mtoto huyu mdogo ndiye mkuu zaidi katika Ufalme wa mbinguni;+ 5 na yeyote anayempokea mtoto mdogo kama huyu kwa msingi wa jina langu ananipokea mimi pia.

  • Luka 9:46-48
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 46 Kisha wanafunzi wakaanza kubishana kuhusu aliyekuwa mkuu zaidi kati yao.+ 47 Yesu, akijua mawazo ya mioyo yao, akachukua mtoto na kumsimamisha kando yake, 48 akawaambia: “Yeyote anayempokea mtoto huyu kwa msingi wa jina langu ananipokea mimi pia, na yeyote anayenipokea, anampokea pia Yule aliyenituma.+ Kwa maana anayejiendesha kama mdogo zaidi kati yenu nyote ndiye mkuu.”+

  • Luka 22:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Hata hivyo, pia kukatokea bishano kali kuhusu ni nani aliyekuwa mkuu zaidi kati yao.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki