-
Mathayo 26:63-65Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
63 Lakini Yesu akakaa kimya.+ Basi kuhani mkuu akamwambia: “Ninakuapisha mbele za Mungu aliye hai utuambie kama wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu!”+ 64 Yesu akamjibu: “Wewe mwenyewe umesema. Lakini ninawaambia: Tangu sasa mtamwona Mwana wa binadamu+ akiwa ameketi kwenye mkono wa kuume wa nguvu,+ akija juu ya mawingu ya mbinguni.”+ 65 Ndipo kuhani mkuu akayararua mavazi yake ya nje, akisema: “Amekufuru! Tunahitaji mashahidi wengine wa nini? Tazama! Sasa mmemsikia akikufuru.
-