11 Mimi ninawabatiza kwa maji kwa sababu mmetubu,+ lakini yule anayekuja baada yangu ana nguvu kuliko mimi, nami sistahili kuvivua viatu vyake.+ Yeye atawabatiza ninyi kwa roho takatifu+ na kwa moto.+
45 Nao waamini* waliotahiriwa ambao walikuwa wamekuja pamoja na Petro wakashangaa, kwa sababu zawadi ya bure ya roho takatifu ilikuwa ikimiminwa pia juu ya watu wa mataifa.
5 Waliposikia hivyo, wakabatizwa katika jina la Bwana Yesu. 6 Paulo alipoweka mikono juu yao, wakapokea roho takatifu,+ nao wakaanza kuzungumza kwa lugha za kigeni na kutoa unabii.+