Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Matendo 4:29, 30
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Na sasa, Yehova,* angalia vitisho vyao, nawe uwawezeshe watumwa wako waendelee kutangaza neno lako kwa ujasiri wote, 30 huku ukinyoosha mkono wako ili uponye, na huku ishara na mambo ya ajabu* yakitukia+ kupitia jina la mtumishi wako mtakatifu Yesu.”+

  • Matendo 6:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Sasa Stefano, akiwa amejaa kibali cha Mungu na nguvu, alikuwa akifanya mambo makubwa ya ajabu* na ishara kati ya watu.

  • Matendo 14:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Basi wakatumia muda mrefu wakizungumza kwa ujasiri kwa mamlaka ya Yehova,* aliyetoa ushahidi kuhusu neno la fadhili zake zisizostahiliwa kwa kuwaruhusu wafanye ishara na mambo ya ajabu.*+

  • Matendo 15:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Ndipo kikundi chote kikanyamaza na kuanza kuwasikiliza Barnaba na Paulo wakisimulia ishara nyingi na mambo ya ajabu* ambayo Mungu alifanya kupitia kwao miongoni mwa mataifa.

  • Waroma 15:18, 19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Kwa maana sitathubutu kusema kuhusu chochote isipokuwa yale ambayo Kristo amefanya kupitia mimi ili mataifa yatii, kwa maneno na matendo yangu, 19 kwa nguvu za ishara na mambo ya ajabu,*+ kwa nguvu za roho ya Mungu, hivi kwamba kutoka Yerusalemu na kuzunguka mpaka Ilirikamu nimehubiri kikamili habari njema kuhusu Kristo.+

  • 2 Wakorintho 12:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Kwa kweli, ishara za mtume zilitokezwa kati yenu kwa uvumilivu mkubwa,+ na kwa ishara na mambo ya ajabu* na matendo yenye nguvu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki