Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Matendo 22:6-11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 “Lakini nilipokuwa safarini nikikaribia kufika Damasko, karibu katikati ya mchana, ghafla nuru kubwa kutoka mbinguni ikamulika kunizunguka,+ 7 nami nikaanguka chini na kusikia sauti ikiniuliza: ‘Sauli, Sauli, kwa nini unanitesa?’ 8 Nikajibu: ‘Wewe ni nani Bwana?’ Naye akaniambia: ‘Mimi ni Yesu Mnazareti, ambaye unamtesa.’ 9 Basi watu waliokuwa pamoja nami, waliiona ile nuru lakini hawakuisikia sauti ya yule aliyezungumza nami. 10 Ndipo nikamuuliza: ‘Nifanye nini Bwana?’ Bwana akaniambia: ‘Simama, uende Damasko, na huko utaambiwa kila kitu ambacho umepangiwa kufanya.’+ 11 Lakini kwa kuwa sikuweza kuona chochote kwa sababu ya utukufu wa nuru hiyo, wale waliokuwa pamoja nami wakanishika mkono na kuniongoza mpaka Damasko.

  • Matendo 26:13-18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 katikati ya mchana niliona barabarani, ewe Mfalme, nuru kutoka mbinguni inayozidi mwangaza wa jua ikimulika kunizunguka mimi na wale waliokuwa wakisafiri pamoja nami.+ 14 Sisi sote tulipoanguka chini, nikasikia sauti ikiniambia katika lugha ya Kiebrania: ‘Sauli, Sauli, kwa nini unanitesa? Kuendelea kuipiga teke michokoo* kunafanya iwe vigumu kwako.’⁠ 15 Lakini nikauliza: ‘Wewe ni nani Bwana?’ Naye Bwana akajibu: ‘Mimi ni Yesu, ambaye unamtesa. 16 Hata hivyo, inuka usimame kwa miguu yako. Kwa sababu nimekutokea ili nikuchague uwe mtumishi na shahidi wa mambo ambayo umeona na pia mambo nitakayokuonyesha kunihusu.+ 17 Nami nitakuokoa kutoka kwa watu hawa na kutoka kwa mataifa ambayo ninakutuma kwao+ 18 ili kuwafungua macho,+ kuwageuza watoke gizani+ waingie kwenye nuru+ na watoke kwenye mamlaka ya Shetani+ wamgeukie Mungu, ili wasamehewe dhambi zao+ na kupata urithi miongoni mwa wale waliotakaswa kwa kuniamini mimi.’

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki