6Basi Yehova akamwambia Musa: “Sasa utaona mambo nitakayomtendea Farao.+ Mkono wenye nguvu utamlazimisha awaruhusu watu wangu waende zao, na mkono wenye nguvu utamlazimisha awafukuze kutoka katika nchi yake.”+
6 “Kwa hiyo, waambie Waisraeli: ‘Mimi ni Yehova, nami nitawatoa kutoka chini ya mizigo ya Wamisri na kuwaokoa kutoka katika utumwa wao,+ nami nitawakomboa kwa mkono ulionyooshwa* na kwa hukumu kubwa.+
6 Kwa maana ninyi ni watu watakatifu kwa Yehova Mungu wenu, na Yehova Mungu wenu amewachagua ninyi muwe watu wake, mali yake ya pekee,* kutoka kati ya mataifa yote yaliyo duniani.+
8 Badala yake, ni kwa sababu Yehova anawapenda na alitimiza kiapo alichowaapia mababu zenu,+ ndiyo maana Yehova aliwatoa Misri kwa mkono wake wenye nguvu na kuwakomboa kutoka katika nyumba ya utumwa,+ kutoka katika nguvu za* Farao mfalme wa Misri.