23Kisha umati huo wote ukasimama na kumpeleka Yesu kwa Pilato.+2 Ndipo wakaanza kumshtaki,+ wakisema: “Tulimkuta mtu huyu akipindua taifa letu na kuwakataza watu wasimlipe Kaisari kodi,+ akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo mfalme.”+
12 Kwa sababu hiyo, Pilato akaendelea kutafuta njia ya kumfungua, lakini Wayahudi wakasema kwa sauti kubwa: “Ukimfungua mtu huyu, wewe si rafiki ya Kaisari. Kila mtu anayejifanya mfalme anasema vibaya kumhusu* Kaisari.”+