46 naye akawaambia: “Imeandikwa kwamba Kristo atateseka na kufufuliwa kutoka kwa wafu siku ya tatu,+47 na kwa msingi wa jina lake, toba kwa msamaha wa dhambi+ ingehubiriwa katika mataifa yote+—kuanzia Yerusalemu.+48 Ninyi mtakuwa mashahidi wa mambo haya.+
8 Lakini roho takatifu itakapokuja juu yenu mtapokea nguvu,+ nanyi mtakuwa mashahidi+ wangu katika Yerusalemu,+ katika Yudea yote na Samaria,+ na mpaka sehemu ya mbali zaidi* ya dunia.”+