Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 12:1-3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Yehova akamwambia Abramu: “Ondoka katika nchi yako na kutoka kwa watu wako wa ukoo na nyumba ya baba yako uende katika nchi nitakayokuonyesha;+ 2 Nitakufanya kuwa taifa kubwa, nami nitakubariki, nami nitalifanya jina lako liwe kuu, nawe utakuwa baraka.+ 3 Nitawabariki wale wanaokubariki, nami nitawalaani wale wanaokulaani,+ na familia zote duniani hakika zitabarikiwa* kupitia kwako.”+

  • Mwanzo 17:5, 6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Jina lako halitakuwa tena Abramu;* jina lako litakuwa Abrahamu,* kwa sababu nitakufanya kuwa baba wa mataifa mengi. 6 Nitakufanya uwe na wazao wengi, wengi sana, nami nitakufanya uwe mataifa, na wafalme watatoka kwako.+

  • Mwanzo 22:17, 18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 hakika nitakubariki, nami hakika nitaufanya uzao* wako uwe mwingi kama nyota za mbinguni na kama chembe za mchanga kwenye ufuo wa bahari,+ na uzao* wako utamiliki lango la* maadui wake.+ 18 Na kupitia uzao wako*+ mataifa yote ya dunia yatajipatia baraka kwa sababu umeisikiliza sauti yangu.’”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki