-
Ufunuo 5:9, 10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Nao wanaimba wimbo mpya,+ wakisema: “Wewe unastahili kukichukua kile kitabu cha kukunjwa na kufungua mihuri yake, kwa sababu ulichinjwa na kwa damu yako ukamnunulia Mungu watu+ kutoka katika kila kabila na lugha na watu na taifa,+ 10 na ukawafanya kuwa ufalme+ na makuhani kwa Mungu wetu,+ nao watatawala wakiwa wafalme+ juu ya dunia.”
-
-
Ufunuo 20:4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Nami nikaona viti vya ufalme, na wale walioketi kwenye viti hivyo wakapewa mamlaka ya kuhukumu. Ndiyo, niliona nafsi* za wale waliouawa* kwa sababu ya ushahidi waliotoa kumhusu Yesu na kwa sababu ya kusema kumhusu Mungu, na wale ambao hawakumwabudu yule mnyama wa mwituni au sanamu yake na ambao hawakupokea ile alama kwenye paji la uso wao na kwenye mkono wao.+ Nao wakawa hai na kutawala wakiwa wafalme pamoja na Kristo+ kwa miaka 1,000.
-