-
Ufunuo 13:15-17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Naye akaruhusiwa kuipa pumzi* ile sanamu ya mnyama wa mwituni, ili ile sanamu ya mnyama wa mwituni iweze kusema na pia kufanya wale wote wanaokataa kuiabudu ile sanamu ya mnyama wa mwituni wauawe.
16 Anawalazimisha watu wote—wadogo kwa wakubwa, matajiri kwa maskini, walio huru kwa watumwa—ili wote watiwe alama kwenye mkono wao wa kulia au kwenye paji la uso wao,+ 17 na ili yeyote asiweze kununua au kuuza isipokuwa mtu aliye na ile alama, jina+ la yule mnyama wa mwituni au namba ya jina lake.+
-